Ukumbini najongea, Kwa kitambo nimemezea,
Mengi nimejionea, Baharini yalojitokezea,
Dunia imejichokea, Kwa binadamu ni mazoea,
Lamba lamba kama asali, cha mwiko utakiona;
Ujio huu sio wa ukali, bali kwa kile nlichokiona,
Uvumi umekuwa kauli, Kwamba sicho wanachokinena,
Wewe umsafi kiakili, mpaka kimwili unajivuna,
Lamba lamba kama asali, cha mwiko utakiona;
Nakuasa wewe baba wawili, Mwenye tamaa za kimwili,
Hivi kweli unaakili, Watoto wa wenzio kuwaingilia kimwili,
Usijione unamali, Tukikuchoka tutakuletea timbwili,
Lamba lamba kama asali, cha mwiko utakiona;
Chezea wa wenzako, Ila siku watu watakuweza,
Siombei mabaya kwako, Bali nakupa ili kukujuza,
Siku tutakukalia kitako, Kama ulezi tutakutandaza,
Lamba lamba kama asali, cha mwiko utakiona;
Yangu mimi namemaliza, Ujumbe umeupata,
Kama shari ishaanza, Kwa kweli utaipata,
Sinashaka utajilaza, Ukitafakari yatayokupata,
Lamba lamba kama asali, cha mwiko utakiona.
Imeandaliwa na Baharia
No comments:
Post a Comment