Maji yana rangi ya tope, na hayapatikani nchini kote,
Maji yamejazwa vyombo vyote, hamna hata cha kuwekea matoke,
Hawasemi lini watayaachia yatoke, japo nguo za ofisi zioshwe,
Leo ni siku ya maji duniani, tuikemee au tuisherehekee?
Wakina mama na watoto foleni bombani,Huku maneno wakirushiana hadharani,
Siku ya pili leo hawajaenda shuleni,Wanawasaidia wazazi kisimani,
Adha hii inajulikana serikalini, wakulitatua hatujui ni nani?
Leo ni siku ya maji duniani, tuikemee au tuisherehekee?
Wengine wanaoshea magari, wengine wamwagilia bustani,
Wengi hawana hata ya kutia kinywani, wengine hawajawahi tia bomba
machoni,
Maji bidhaa adimu sio vijijini tu bali hata mijini, na hatujui yataisha
lini?
Labda tutumie ya baharini kwa matumizi ya nyumbani,
Leo ni siku ya maji duniani, tuikemee au tuisherehekee?
Imeandaliwa na Ally Bukuku/Buchicks
No comments:
Post a Comment